Friday, September 20, 2013

SIO WASIKIAO, BALI WATENDAO.



SIO WASIKIAO, BALI WATENDAO.

1.      Ni kwa nini ahadi ilipewa Ibrahimu ya kuwa yeye na uzao wake watairithi nchi?
Kwa sababu Ibrahimu alisikia sauti yangu,akayahifadhi maagizo yangu,na amri zangu,na hukumu zangu,na sheria zangu.” Mwanzo 26:5.

  1. Ni na nani ndio Bwana ataweka agano, na kumuonyesha rehema?
Basi jueni ya kuwa BWANA,Mungu wenu,ndiye Mungu;Mungu mwaminifu,ashikaye agano lake na rehema kwao wampendao,na kushika amri zake hata vizazi elfu.” Kumbukumbu la Torati 7:9.

  1. Ni kwa nani ndiyyo Kristo anaelezea baraka?
       Lakini yeye alisema, Afadhali, heri walisikiao neno la Mungu na kulishika.” Luka 11:28.

  1. Je wote wasemao,’Bwana, Bwana’ wtaokolewa mwishowe?
     Si kila mtu aniambiaye, Bwana, Bwana, atakayeingia katika ufalme wa mbinguni;” Mathayo 7:21.

  1. Basi nani ataruhusiwa kuingia?
Si kila mtu aniambiaye, Bwana, Bwana, atakayeingia katika ufalme wa mbinguni; bali ni yeye afanyaye mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni.” Mathayo 7:21.

  1. Ni visababu gani wengi watatoa katika siku hiyo kuu?
“Wengi wataniambia siku ile, Bwana, Bwana, hatukufanya unabii kwa jina lako, na kwa jina lako kutoa pepo, na kwa jina lako kufanya miujiza mingi?” Mathayo 7:22.

  1. Ni jibu gani watapokea?
Ndipo nitawaambia dhahiri, Sikuwajua ninyi kamwe; ondokeni kwangu, ninyi mte­ndao maovu.” Mathayo 7:23.

  1. Watiifu wamefananishwa na nini?
“Basi kila asikiaye hayo maneno yangu, na kuyafanya, atafananishwa na mtu mwenye akiIi, aliyejenga nyumba yake juu ya mwamba.” Mathayo 7:24.

  1. Wale wasikiao neno, bali hushindwa kutii wamefananishwa na nini?
Na kila asikiaye hayo maneno yangu asiyafanye, atafananishwa na mtu mpumbavu, aliyejenga nyumba yake juu ya mchanga.” Mathayo 7:26.

  1. Ni nani ndio Paulo anasema watahesabiwa haki?
Kwa sababu sio wale waisikiao sheria walio wenye haki mbele za Mungu, bali ni wale waitendao sheria watakaohesabiwa haki.” Warumi 2:13.


KUAMINI KATIKA YESU.



KUAMINI KATIKA YESU.

  1. Nini ndio nabii wa Agano la kale alitabiri kuhusu Kristo? 
Isaya 11:10.

  1. Ni vipi mtume alielezea unabii huu?
Na tena lsaya anena, Litakuwako shina la Yese, Naye aondokeaye kuwatawala Mataifa; Ndiye Mataifa watakayemtumaini.” Warumi 15:12.

  1. Mitume waliomuamini Kristo kwanza, walikuwa wawe akina nani?
Nasi katika huyo tupate kuwa sifa ya utukufu wake, sisi tuliotangulia kumwekea Kristo tumaini letu.” Waefeso 1:12.

  1. Nini ndio Waefeso walifanya waliposikia ujumbe wa kweli?
“Nanyi pia katika huyo mmekwisha kulisikia neno la kweli, habari njema za wokovu wenu; tena mmekwisha kumwamini yeye, na kutiwa muhuri na Roho yule wa ahadi aliye MtakatifuFungu la 13,sehemu ya kwanza.

  1. Ni matokeo gani walipokea kutokana na ukweli waliouamini?
     “Nanyi pia katika huyo mmekwisha kulisikia neno la kweli, habari njema za wokovu wenu; tena mmekwisha kumwamini yeye, na kutiwa muhuri na Roho yule wa ahadi aliye MtakatifuFungu la 13,sehemu ya mwisho.

  1. Ni kwa nani ndio injili inakuwa nguvu za Mungu?
Kwa maana siionei haya Injili; kwa sababu ni uweza wa Mungu uuletao wokovu, kwa kila aaminiye,                      kwa Myahudi kwanza, na kwa Myunani pia.” Warumi 1:16.

  1. Na ikiwa mtu atasitasita katika imani yake au kuamini; anachukuliwaje na Bwana?
Lakini mwenye haki wangu ataishi kwa imani; Naye akisita-sita, roho yangu haina furaha naye.” Waebrania 10:38.

  1. Ni kupitia kwa nini ndio mtu anapata ushindi juu ya dunia?
Kwa maana kila kitu kilichozaliwa na Mungu huushinda ulimwengu; na huku ndiko kushinda kuushindako ulimwengu, hiyo imani yetu.” 1 Yohana 5:4.